October 23, 2021

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa umma Fredy Mwakibete amesema kuna haja ya Serikali kuangalia uwezekano wa kutenga fungu katika bajeti yake kwa ajili ya Asasi za Kiraia (AZAKI). Mwakibete ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Busekelo amesema Azaki zinawafikia na kuwasaidia wananchi.....

MBUNGE: Serikali Itenge Fungu kwa Ajili ya AZAKI
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa umma Fredy Mwakibete amesema kuna haja ya Serikali kuangalia uwezekano wa kutenga fungu katika bajeti yake kwa ajili ya Asasi za Kiraia (AZAKI).

Mwakibete ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Busekelo amesema Azaki zinawafikia na kuwasaidia wananchi wengi ambao wakati mwingine hata Serikali kuwafikia ni vigumu.

“Asasi za kiraia zinakwenda moja kwa moja kwa wananchi hata pale ambapo Serikali imeshindwa kufika nyie mnafika na mnagusa makundi yote katika Jamii ikiwemo wanawake na walemavu,” amesema Mwakibete akirejea Mchango wa Taasisi ya HakiRasimali ambayo imetoa elimu kwa watu wengi kuhusu sekta ya Uziduaji.

Amesema kutokana na mchango huo wa asasi hizo Serikali haina budi kuwa na fungu maalumu kwa ajili ya kuwaunga mkono na kuwawezesha kufika kule ambako kwao isingekuwa rahisi kufika.

Related Posts

Call for Application-Extractive Sector Knowledge Transfer Incubator (ESKi)
Sep 02, 2025

Call for Application-Extractive Sector Knowledge Transfer Incubator (ESKi)

ESKi Tanzania ni programu ya kukuza uwezo iliyoundwa ili kukuza na kuendeleza kizazi kipya cha viongozi, watetezi wa jamii na wataalamu wanaoshughulik...

Call for Application – Extractive Sector Knowledge Transfer Incubator (ESKi)
Sep 01, 2025

Call for Application – Extractive Sector Knowledge Transfer Incubator (ESKi)

Capacity-building opportunity for CSOs, youth and media to deepen technical expertise.

External audit services tender
Aug 14, 2025

External audit services tender

HakiRasilimali invites qualified firms to submit proposals for annual audit engagements.