November 09, 2023

Afshin Nazir, Afisa sera na uchechemzi wa AFRODAD: "Afrika ni bara tajiri na masikini wakati huohuo tunazo rasilimali nyingi za kutufanya tuwe matajiri lakini bado tunaishi katika umasikini mkubwa" Nazir amesema sababu kubwa ya umasikini barani Afrika ni kukosekana kwa mikakati na usimamizi madhubut...

Afrika ni bara tajiri na masikini wakati huohuo tunazo rasilimali nyingi za kutufanya tuwe matajiri lakini bado tunaishi katika umasikini mkubwa
Afshin Nazir, Afisa sera na uchechemzi wa AFRODAD: "Afrika ni bara tajiri na masikini wakati huohuo tunazo rasilimali nyingi za kutufanya tuwe matajiri lakini bado tunaishi katika umasikini mkubwa" Nazir amesema sababu kubwa ya umasikini barani Afrika ni kukosekana kwa mikakati na usimamizi madhubuti wa rasilimali zilizopo. Amezungumzia athari za madeni katika kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi akisema changamoto ya madeni kwa nchi yanakwaza juhudi zote muhimu.

"Mataifa mengi ya Afrika yanatumia kiasi kikubwa cha mapato yake kulipa madeni kwa kuwa yanadaiwa fedha nyingi lakini tukiwa na mikakati mizuri tunaweza kutumia rasilimali zetu kugharimia mambo yote muhimu ikiwemo kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi" Vilevile amesema kutokana na kutokuwa na mikakati madubuti Afrika inakosa sauti katika majukwaa ya mabadiliko ya tabianchi duniani licha ya kuwa ni mdau namba moja katika safari hiyo.

Related Posts

Call for Application-Extractive Sector Knowledge Transfer Incubator (ESKi) 2026
Jul 21, 2026

Call for Application-Extractive Sector Knowledge Transfer Incubator (ESKi) 2026

About the Programme ESKi Tanzania is a capacity development programme designed to nurture and empower the next generation of leaders, community advoca...

CALL FOR ABSTRACTS
Jun 12, 2026

CALL FOR ABSTRACTS

📢 CALL FOR ABSTRACTS HakiRasilimali invites researchers, academics, practitioners, policymakers, and civil society actors to submit abstracts for th...

Call for Application-Extractive Sector Knowledge Transfer Incubator (ESKi)
Sep 02, 2025

Call for Application-Extractive Sector Knowledge Transfer Incubator (ESKi)

ESKi Tanzania ni programu ya kukuza uwezo iliyoundwa ili kukuza na kuendeleza kizazi kipya cha viongozi, watetezi wa jamii na wataalamu wanaoshughulik...